MWANAMUZIKI
Nguza Vicking ‘Babu Seya’ na mwanaye, Johnson Nguza ‘Papii Kocha’ ambao
wanasota jela kwa kosa la kuwanajisi watoto 9, wamedaiwa kusaka
uwezekano wa kujinasua gerezani kwa kumuangukia Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli.
Taarifa
kutoka kwa chanzo makini zimeeleza kuwa wanamuziki hao kwa kushirikiana
na ndugu zao, wamemuandikia barua binafsi rais ili aweze kusikia kilio
chao na ikiwezekana wasamehewe kutokana na mamlaka aliyo nayo.
“Si
unakumbuka kipindi kile waliwahi kumuandikia waraka JK (Jakaya Kikwete,
rais wa awamu ya nne) kumuomba awasamehe lakini bahati mbaya maombi yao
hayakuzaa matunda! Wameona wajaribu kwa Magufuli ili ikiwezekana
kupitia ile sheria inayompa mamlaka rais kusamehe mtu yeyote
aliyehukumiwa kwa kosa lolote, awasamehe kina Babu Seya,
“Nasikia
wameshaandika barua, wanaipeleka ikulu na wana imani Magufuli ni mtu
anayeguswa sana na hofu ya Mungu, huenda akawasamehe,” kilisema chanzo
hicho.
Alipotafutwa
mtoto mkubwa wa Babu Seya, Mbangu Nguza na kuulizwa kama wamepeleka
barua hiyo na matumaini ya ndugu zake kutoka gerezani, hakutaka kukubali
au kukataa lakini akasema wao wana imani muda wowote ndugu zao watatoka
gerezani.
“Kila
siku nimekuwa nikisisitiza hili suala, labda niseme tena, Babu Seya na
Papii watatoka siku si nyingi kutoka sasa,” alisema Mbangu.
Amani
liliwasiliana na Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Gerson Msigwa
na kumuuliza kama wamepokea barua hiyo, alisema hawajaipata na kuomba
apewe muda afuatilie na atatoa majibu.
“Sijaiona hiyo barua, ngoja nitafuatilia na nitakujulisha,” alisema Msigwa.
KUMBUKUMBU
Juni
25, 2004, Hakimu Mkuu Mkazi wa Mahakama ya Kisutu, Dar es Salaam, Addy
Lyamuya aliwatia hatiani Babu Seya na wanaye watatu, Papii Kocha, Mbangu
na Francis.
Januari
27, 2005, Jaji wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, Thomas Mihayo
alitupilia mbali rufaa yao iliyokuwa ikipinga hukumu hiyo.
Wakili
wao, Mabere Nyaucho Marando akapeleka suala hilo Mahakama ya Rufaa
Tanzania ambako Mbangu na Francis waliachiwa huru, Babu Seya na Papii
wakaonekana bado wana hatia.
Babu
Seya na wanaye walidaiwa kutenda makosa 10 ya kubaka na kulawiti watoto
hao kati ya Aprili na Oktoba, 2003 katika maeneo ya Sinza ya Palestina,
Dar es Salaam. Mpaka sasa wana miaka 12 Gerezani
Post a Comment