Viungo wakabaji, Jonas Mkude na Justice Majabvi wana kila dalili za kutokuwemo katika kikosi cha Simba msimu ujao.
Mkude yupo nchini Afrika Kusini kwa majaribio katika moja ya klabu ya ligi kuu nchini humo. Kiungo huyo aliondoka nchini wiki iliyopita kujaribu bahati yake kwa mara ya pili baada ya awali kufanya hivyo na kukosa nafasi katika klabu ya Bidvest Wits.
Majabvi, raia wa Zimbabwe ambaye alikuwa moja ya nguzo muhimo katika kuikinga safu ya ulinzi msimu uliopita yupo katika mipango ya kuhamia nchini Austria alikowahi kucheza soka la kulipwa.
kikosi cha Simba kimeagwa hii leo na mashabiki, viongozi na wanachama tayari kuelekea mkoani Morogoro kupiga kambi kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya wa Ligi Kuu.
Post a Comment