Mshambuliaji Laudit Mavugo, raia wa Burundi ametajwa kuwa mchezaji bora wa mwezi wa kwanza wa klabu ya Simba.
Hii ni mara ya kwanza kwa Mavugo kutwaa tuzo hio inayotolewa kila mwezi kwa mchezaji wa Simba aliyeonesha mchango mkubwa zaidi.
Baada ya kusuasua kwa muda mrefu, Mavugo alifanikiwa kufunga katika mechi nne zmfululizo zilizopita kiasi cha kurudisha matumaini kwa mashabiki waliokuwa na matarajio makubwa kwake alipotua nchini mwanzoni mwa msimu huu.