banner

March 15, 2017

WAAJIRI NA WATUMISHI WA UMMA NCHINI: OPRAS IPO KWA SHERIA HIVYO NI WAJIBU KUITEKELEZA IPASAVYO.

WAAJIRI NA WATUMISHI WA UMMA NCHINI: OPRAS IPO KWA SHERIA HIVYO NI WAJIBU KUITEKELEZA IPASAVYO.

Mkurugenzi wa Idara ya Uchambuzi na Ushauri wa Kazi, Ofisi ya Rais-Utumishi, Bw. Mick Kiliba (wa kwanza kulia) akizungumza mapema leo katika kipindi cha JAMBO kinachotangazwa na TBC One kuhusu Mfumo wa Wazi wa Mapitio na Tathmini ya Utendaji Kazi (OPRAS). Wengine katika picha ni Mkurugenzi Msaidizi, Sehemu ya Mifumo na Viwango vya Utendaji Kazi kutoka Ofisi ya Rais – Utumishi, Bi. Veila Shoo (katikati) na Mwongozaji wa kipindi hicho, Bw. Rashid Salim.
MWAKI2
Mtangazaji wa Kipindi cha “JAMBO” kinachotangazwa na TBC One, Bw. Rashid Salim (kushoto) katika mahojiano na Mkurugenzi wa Idara ya Uchambuzi na Ushauri wa Kazi wa Ofisi ya Rais-Utumishi, Bw. Mick Kiliba, pamoja na Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Mifumo na Viwango vya Utendaji Kazi kutoka Ofisi ya Rais – Utumishi, Bi. Veila Shoo. Kipindi cha Jambo maudhui yake yalikua kutoa elimu kuhusu umuhimu wa Mfumo wa Wazi wa Mapitio na Tathmini ya Utendaji Kazi (OPRAS) kwa Waajiri na Watumishi wa Umma nchini.
MWAKI3
Mkurugenzi wa Idara ya Uchambuzi na Ushauri wa Kazi wa Ofisi ya Rais-Utumishi, Bw. Mick Kiliba (kulia) akifafanua jambo kuhusu umuhimu wa Mfumo wa Wazi wa Mapitio na Tathmini ya Utendaji Kazi (OPRAS) kwa Waajiri na Watumishi wa Umma mapema leo katika kipindi cha JAMBO kinachotangazwa na TBC Taifa. Kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Mifumo na Viwango vya Utendaji Kazi kutoka Ofisi ya Rais – Utumishi, Bi. Veila Shoo. Wengine ni waongozaji wa kipindi hicho, Bi. Anna Mwasyoke na Bw. Paul Alphonce.
MWAKI4
Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Mifumo na Viwango vya Utendaji Kazi kutoka Ofisi ya Rais – Utumishi, Bi. Veila Shoo (kushoto) akizungumza mapema leo katika kipindi cha JAMBO kinachotangazwa na TBC Taifa kuhusu umuhimu wa Mfumo wa Wazi wa Mapitio na Tathmini ya Utendaji Kazi (OPRAS) kwa Waajiri na Watumishi wa Umma nchini. Kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Uchambuzi na Ushauri wa Kazi wa Ofisi ya Rais-Utumishi, Bw. Mick Kiliba. Wengine ni waongozaji wa kipindi hicho kushoto ni Bi. Anna Mwasyoke na Bw. Paul Alphonce.

Post a Comment

Whatsapp Button works on Mobile Device only

Start typing and press Enter to search