banner

July 26, 2017

DAKTARI WA YANGA AMFANYIA VIPIMO KABAMBA TSHISHIMBI

DAKTARI WA YANGA AMFANYIA VIPIMO KABAMBA TSHISHIMBI

Kiungo wa Mbambane Swallows aliyekuwa akisakwa kwa nguvu kubwa na Klabu ya Yanga, Kabamba Tshishimbi amefanyiwa vipimo vya afya na inavyoonekana suala la kusaini mkataba mpya klabuni hapo lipo njiani.
Kabamba ambaye ni raia wa DRC Congo aliyekuwa akikipiga katika Klabu ya Mbambane Swallows ya Swaziland ameonekana akifanyiwa vipimo vya afya na Daktari Nassor Matuzya.
Katika picha hizo kiungo huyo anaonekana akipimwa pia urefu na baadaye kumshukuru Matyuza ambaye amekuwa akifanya kazi karibu na Klabu ya Yanga na amewahi kuwa daktari rasmi wa klabu hiyo mara kadhaa kipindi cha nyuma.

Post a Comment

Whatsapp Button works on Mobile Device only

Start typing and press Enter to search