banner

July 26, 2017

MATOLA KAAMUA, ATEMA WACHEZAJI 10, ASAJILI 10 LIPULI FC

MATOLA KAAMUA, ATEMA WACHEZAJI 10, ASAJILI 10 LIPULI FC

Kocha mpya wa Lipuli FC, Selemani Matola amezungumza juu ya mikakati yake ya kuijenga upya timu hiyo ambapo amesema ana mipango ya kuongeza wachezaji 10 wapya.
Matola ambaye ni kiungo na kocha wa zamani wa Simba, amesema kuwa usajili huo wa wachezaji 10 unatokana ripoti ya kocha aliyepita ambayo aliikabidhi klabuni hapo.
Amesema kutakuwa na wachezaji 10 wapya, pia walioipandisha timu nao watabaki 10 na wachezaji watano watapatikana kutokana na majaribio ambayo wamekuwa wakiyafanya kikosini hapo.
Hivyo, jumla Lipuli FC itakuwa na wachezaji 25 katika msimu ujao wa 2017/18, lakini amedai kuwa usajili huo utategemea na mwongozo wa uongozi wake wa Lipuli FC.

Post a Comment

Whatsapp Button works on Mobile Device only

Start typing and press Enter to search