banner

July 26, 2017

MSUVA KUONDOKA DAR JUMATANO HII KUELEKEA MOROCCO

MSUVA KUONDOKA DAR JUMATANO HII KUELEKEA MOROCCO

Winga wa Yanga, Simon Msuva anatarajiwa kuondoka jijini Dar es Salaam, Jumatano ya Julai 26 kwa ajili ya kwenda nchini Morocco kukamilisha mchakato wa uhamisho wake kujiunga na timu ya Difaa Hassani El-Jadida inayoshiriki Ligi Kuu ya Morocco.
Difaa ambayo imeshamsajili Mtanzania mwingine, Ramadhani Singano kutoka Azam FC, iko tayari kutoa dola 150,000 kumsajili Msuva ambaye amebakiza miezi tisa katika mkataba wake Yanga.
Imeelezwa kuwa Msuva ameshafuzu vipimo vya afya na akifika Morocco anatarajiwa kusaini moja kwa moja mkataba wa kujiunga na timu hiyo.
Msuva alishindwa kwenda Morocco tangu wiki jana kwa kuwa alikuwa Kigali, Rwanda kwa ajili ya majukumu ya timu ya taifa ya Tanzania uliyokuwa ikiwania tiketi ya kucheza michuano ya Afrika kwa Wachezaji Wanaocheza Ligi za Ndani (CHAN). 

Post a Comment

Whatsapp Button works on Mobile Device only

Start typing and press Enter to search