banner

July 26, 2017

REAL MADRID KUWEKA KUFURU KWA MBAPPE, WAKUBALI KUMSAJILI KWA PAUNI 160M

REAL MADRID KUWEKA KUFURU KWA MBAPPE, WAKUBALI KUMSAJILI KWA PAUNI 160M

Inadaiwa Real Madrid imekubali kumsajili Kylian Mbappe kutoka Monaco kwa pauni 160m, italipa pauni 143, kisha 17m itakuwa nyongeza katika mkataba.
Ikiwa taarifa hizo zitakuwa na ukweli na dili hilo litakamilika, inamaana kuwa kuna Real Madrid itakuwa inaandika rekodi ya kuwa klabu iliyotoa fedha nyingi kusajili mchezaji mmoja.
Rekodi ya sasa ya mchezaji aliyesajiliwa kwa dau kubwa duniani inashikiliwa na Paul Pogba ambaye alisajiliwa kwa pauni milioni 89 kutoka Juventus kwenda Manchester United.
Mbappe amekuwa akiwindwa na klabu nyingi kubwa za Ulaya, hivyo kama ni kweli Madrid wanataka kuweka dau hilo, inamaanisha kuwa wamezifukuza klabu zote katika dili hilo ili wabaki wao tu. 

Post a Comment

Whatsapp Button works on Mobile Device only

Start typing and press Enter to search