Kikosi cha Yanga kinatarajiwa kuondoka jijini Dar es Salaam mchana wa leo Jumatano kuelekea Morogoro kwa ajili ya kuendeleza mchakato wa kujiandaa kwa msimu ujao wa 2017/18.
Yanga ambao ni mabingwa hao wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara wanatarajiwa kuwa kambini mkoani Morogoro kwa muda wa siku saba kujiandaa na michezo miwili ya kirafiki itakayopigwa Agosti 6 na 12, mwaka huu.
Ofisa Habari wa Yanga, Dismass Ten amethibitisha juu ya safari hiyo kwa kusema kocha wao mkuu, George Lwandamina anatarajiwa kuitumia kambi hiyo kukiandaa kikosi chake vizuri ambapo msimu huo unaokuja kinatarajiwa kushiriki katika Ligi ya Mabingwa Afrika.
Post a Comment