banner

October 01, 2018

ZIDANE, MOURINHO, SANCHEZ, RONALDO: TETESI KUBWA ZA SOKA ULAYA LEO JUMATATU

ZIDANE, MOURINHO, SANCHEZ, RONALDO: TETESI KUBWA ZA SOKA ULAYA LEO JUMATATU

Meneja wa Manchester United Jose Mourinho ana hofu kuhusu hatma yake huko Old Trafford na anaamini kuwa maafisa wa klabu wamewasiliana na meneja wa zamani wa Real Madrid Zinedine Zidane. (Sun)

Lakini mchezaji huyo wa zamani kimataifa wa Ufaransa analenga kuwa meneja mpya wa Juventus. (Tuttosport, via Daily Express)

Sintofahamu kuhusu hatma ya Mourinho huko United inamaanisha kuwa wachezaji 12 hawana uhakika kuhusu hatma yao wakati wanaingia mwaka wa mwesho wa mikataba yao. (Daily Mirror)


Mourinho amekosa uvumilivu kwa mshambuliaji raia wa Chile Alexis Sanchez, 29. (London Evening Standard)

Mlinzi wa Manchester United raia wa England Luke Shaw, 23, anasema kikosi kilicheza vibaya wakati kilishindwa na West Ham siku ya Jumamosi. (Daily Telegraph)


Manchester City watangoja kabla ya kumpa ofa mpya kiungo wa kati mwenye miaka 18 Phil Foden ya mkataba mpya wa miaka mitano wa pauni 250,000 kwa wiki. (Daily Star)

Meneja wa City Pep Guardiola amemuonya wing'a mjerumani Leroy Sane, 22, akitaka asipoteze mwelekeo. (Sun)


Maajenti wa Manchester City, Liverpool na Tottenham walimtazama kiungo wa kati wa Lazio raia wa Serbia Sergej Milinkovic-Savic, 23, wakati wa ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya Genoa. (Daily Mirror)

AC Milan, Manchester United na Paris Saint-Germain walijaribu kumsaini Cristiano Ronaldo msimu huu kabla ya mreno huyo mwenye miaka 33 kujiunga na Juventus kutoka Real Madrid. (El Mundo, via Marca)
'

Mmiliki wa Newcastle Mike Ashley atapeleka kikosi kizima na menaja Rafa Benitez kwa mlo katika jitihada za kujenga uhusiano. (Daily Mail)

Kutoka BBC

Whatsapp Button works on Mobile Device only

Start typing and press Enter to search