banner

October 10, 2019

HILI NDIYO BALAA LA PYRAMDS FC, WALIITWANGA ETOILE DU CONGO TANO, REKODI ZAO HIZI HAPA

HILI NDIYO BALAA LA PYRAMDS FC, WALIITWANGA ETOILE DU CONGO TANO, REKODI ZAO HIZI HAPA


Timu ilianzishwa miaka 11 iliyopita 2008 ikijulikana Kama Al Assiouty Sport. 2014 walipanda ligi kuu ya Misri,2018 ilinunuliwa na Mwenyekiti wa makampuni ya Saud Sport Authority na kubadilisha jina kutoka Al Assiouty Sport na kua Pyramids FC.

Juni mwaka huu mfanyabiashara toka Emirate Salem Al alifanikiwa kua mmiliki wa timu hii baada ya kununua hisa zote na kuwekeza pesa nyingi.

Kwa Sasa inafundishwa na Kocha Sebastian Desabre aliyewai kua kocha wa timu ya Taifa Uganda 2017-2019 raia wa ufaransa. Ni kocha mzoefu Africa amewai kufundisha vilabu vikubwa barani Africa Kama Esperance ya Tunisia ,Asec mimomasa ,Libolo ,waydad Casablanca Morroco na Ismaily.

Msimu uliopita kwa mara ya kwanza walishika nafasi ya Tatu katika ligi kuu ya Misri nyuma ya mabingwa Al Ahly na Zamaleck hivyo kupata tiketi ya kuwakilisha Misri michuano ya Confederation cup msimu huu.

Hatua ya awali walikutana na Etoile du Congo ya Congo na waliitoa kwa kujumla ya magoli 5-1 mechi ya kwanza Misri wakitoka 4-1 na marudiano Congo wakishinda 1 kwa bila.

Hatua inayofuata walikutana na CR Belouizdad ya Algeria na waliitoa kwa jumla ya magoli 2-1 mechi ya awali nchini Misri wakitoka 1-1 na mechi ya marudiano Pryamids fc wakishinda goli 1 kwa bila na kufuzu hatua ya Play off.

Takwimu zinaonyesha katika michuano hii ya CAF wameshinda mechi zote ugenini na moja nyumbani na kutoka sare moja nyumbani hivyo ni timu inayoweza kutoa matokeo ugenini.

Kocha wa zaman Al Ahly Hossam El Badry ndie Mwenyekiti wa klabu -Msemaji wao pia ni Mchezaji wa zaman Misri.

Ikiwa hii ni mara yao ya kwanza kushiriki michuano chini ya CAF, wanaowachezaji kutoka mataifa mbalimbali ikiwemo John Attwa toka Ghana.



Post a Comment

Whatsapp Button works on Mobile Device only

Start typing and press Enter to search