banner

October 13, 2019

YANGA: TUNAWAPIGA TATU HAPA BONGO HAWA WAARABU

YANGA: TUNAWAPIGA TATU HAPA BONGO HAWA WAARABU


UONGOZI wa Yanga umesema kuwa wapinzani wao Pyramids kutoka Misri wajiandae kuchapwa mabao matatu uwanja wa CCM Kirumba kabla ya marudiano.

Yanga itamenyana na Pyramids Octoba 27 kwenye mchezo wa kwanza wa kimataifa wa kombe la Shirikisho kabla ya kurudiana nao nchini Misri.

Ofisa Uhamasishaji wa Yanga, Antonio Nugaz amesema kuwa wamejipanga kuifunga Pyramids mabao matatu ya haraka kabla ya kuwafuata kwao.

"Tunahitaji kuwafunga mabao matatu fasta kabla ya kuwafuata kwao, tuna kazi kubwa ya kufanya ila inawezekana na hatutawaangusha mashabiki.

"Tunahitaji kupunguza kazi ya kuwafuata tukiwa na mzigo mkubwa ugenini tukianza kuwafunga mabao mengi haa itakuwa rahisi kushinda kwao, huko tutawaiga moja kisha tunaweka ukuta mzito," amesema.


Post a Comment

Whatsapp Button works on Mobile Device only

Start typing and press Enter to search