banner

February 26, 2020

SABABU YA STAND UNITED KUSHINDWA KUFURUKUTA MBELE YA SIMBA YATAJWA

SABABU YA STAND UNITED KUSHINDWA KUFURUKUTA MBELE YA SIMBA YATAJWA

ATUGA Manyundo, Kocha Mkuu wa Stand United amesema kuwa alikutana na kikosi bora cha Simba jambo lililomfanya ashindwe kupenya kwenye mikwaju ya penalti licha ya vijana wake kucheza kwa kujituma kwenye mchezo wa hata ya 16 bora ya Kombe la Shirikisho.

Manyundo alikuwa Kocha Mkuu wa Mashujaa ambao waliitoa Simba msimu uliopita wa mwaka 2018 kwenye hatua ya 62 bora Uwanja wa Taifa jana alipoteza kwa kufungwa kwa mikwaju 3-2 ya penalti mbele ya Simba Uwanja wa Kambarage baada ya dakika 90 kutoshakwa kufungana bao 1-1.

Manyundo amesema:"Nilikuwa ninatambua kwamba ninakutana na timu bora, niliwaambia wachezaji wangu wacheze kwa nidhamu kwa kuwa Simba ninaitambua na tulifanya hivyo mwanzo mwisho.

"Kutolewa kwa changamoto ya penalti kwetu sio mbaya kwani yoyote yule anaweza kutolewa kwa penalti," amesema.


Post a Comment

Whatsapp Button works on Mobile Device only

Start typing and press Enter to search