Leo Uwanja wa Uhuru saa 10:00 Azam FC inayonolewa na Arstica Cioaba raia wa Romania itakuwa kwenye vita ya kuwania pointi tatu na Coastal Union inayonolewa na mzawa Juma Mgunda.
Azam FC iliyo nafasi ya pili na pointi 44, kwenye mechi za mwezi Februari imefunga jumla ya mabao sita na kufungwa mabao matatu huku ikishinda mechi mbili na kulazimisha sare mbili. Kwenye pointi 12 imebeba nane na kuzipeperusha nne.
Matokeo yao yalikuwa namna hii:-Mbeya city 1-1 Azam FC, Feb 2, Azam 1-1 Prisons, Feb 5, Azam 3-1 KMC Feb 8, Azam 1-0 Polisi Tanzania.
Kwa upande wa Coastal Union iliyo nafasi ya sita na pointi 34 imefunga mabao matatu na kufungwa mabao matatu kwenye pointi 12 imeambulia pointi tano na kuzipeperusha saba. Matokeo yao yalikuwa hivi:- Simba 2-0 Coastal Union, Februari Mosi, JKT Tanzania 1-1 Coastal, Feb 04, Coastal Union 2-0 Polisi Tanzania, Februari 8, KMC 0-0 Coastal Union Februari 12.
Post a Comment