banner

April 07, 2020

ISHU YA OKWI KURUDI NDANI YA SIMBA IPO HIVI

ISHU YA OKWI KURUDI NDANI YA SIMBA IPO HIVI

INAELEZWA kuwa uongozi wa Simba upo kwenye mazungumzo na nyota wao wa zamani, Emannuel Okwi ili arejee tena kukipiga kwa mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu Bara.

Okwi kwa sasa anakipiga ndani ya Klabu ya Al Ittihad alijiunga nayo kwa dau la dola 257,000 zaidi ya shilingi milioni 592 akitokea Simba.

Habari zinaeleza kuwa kinachokwamisha dili la nyota huyo kwenda sawa ni mkwanja ambao anauhitaji kuwa mkubwa jambo ambalo linawapasua kichwa mabosi wa Simba.

"Okwi anatakiwa kurudi ndani ya Simba ila ishu kubwa ni mshahara wake ambao anahitaji kulipwa zaidi ya milioni 20 kwa mwezi jambo ambalo bado linajadiliwa.

"Mahitaji yake ni kuona analipwa dola 10,000 (zaidi ya milioni 23) kutokana na hali hiyo uongozi umeona uweke kando kwanza dili hilo," ilieleza taarifa hiyo.

Mtendaji Mkuu wa Simba, Senzo Mazingisa  amesema:" Kwa sasa kocha ametoa mapendekezo yake ya mchezaji wa kusajiliwa na kuachwa, hatuwezi kuweka wazi siri za klabu muda ukifika kila kitu kitajulikana,".

Okwi akiwa Simba ametwaa ubingwa wa Ligi Kuu Bara mara tatu ikiwa ni msimu wa 2011/12,2017/18 na 2018/19.

Chanzo SpotiXtra


Post a Comment

Whatsapp Button works on Mobile Device only

Start typing and press Enter to search