Baada ya kuitwanga Manchester City kwa jumla ya mabao 3-2 katika mchezo wa Ligi Kuu England jana Jumamosi, Kocha wa Manchester United, Jose Mourinho, amesema timu yake inastahili kupewa heshima.
United ilikuwa nyuma kwa mabao 2-0 kabla ya kusawazisha na kuongeza jingine ambalo lilidumu mpaka dakika ya mwisho ya mchezo. Kutokana na matokeo hayo ya ugenini, Mourinho amesema kuwa hakika wachezaji wake walipambana wakiwa ugenini kwa kupindua matokeo baada ya kuwa nyuma kwa bao hizo mbili. "Nadhani tunastahili kupewa heshima, wachezaji wako vizuri nami niko vizuri kuliko watu wanavyofikiria" alisema Mourinho. Katika mchezo huo, Manchester City ilijipatia mabao yake kupitia Vincent Kompany na Gundogan huku United wakifunga kupitia Pogba aliyetia kambani mabao mawili na jingine likifungwa na Smalling.
Na George Mganga Kikosi cha Simba kinafanya mazoezi ya mwisho mjini Morogoro leo, tayari kwa mchezo wa ligi dhidi ya Mtibwa Sugar utakaopigwa mjini Morogoro kesho Jumatatu. Simba na Mtibwa zitakuwa zinaingia Jamhuri zikiwa na kumbukumbu ya kupata matokeo kwenye mechi zilizopita, ambapo Simba iliiadhibu Njombe Mji kwa mabao 2-0 huku Mtibwa ikiilaza vikali Singida United 3-0, michezo yote ikipigwa ugenini. Simba itakuwa kibaruani bila wachezaji wake muhimu watatu ambao wanatumikia adhabu ya kuwa na kadi tatu za njano. Beki Juuko Murushid, Erasto Nyoni na Kiungo James Kotei hawataitumikia timu yao kesho sababu ya kuwa na idadi ya hiyo ya kadi za njano, hivyo watalazimika kuisubiri Tanzania Prisons kwenye unaofuata baada ya Mtibwa Sugar. Licha ya kukosekana wachezaji hao, Kiungo Jonas Mkude anatarajiwa kuwa sehemu ya kikosi kufuatia kupona majeraha yake ya kifundo cha mguu aliyoyapata wiki moja iliyopita wakati timu ikijiandaa na mchezo dhidi ya Njombe Mji. Mkude aliumia kifundo hicho baada ya kukwaana miguu na kiungo mwenzake, Mzamiru Yassin kwenye Uwanja wa Boko Vetarani uliopo pembezoni kidogo mwa jiji la Dar es Salaam.
Na George Mganga Kiungo Mshambuliaji wa klabu ya Yanga, Raphael Daud, jana aliweka rekodi yake katika mashindano ya Kombe la Shirikisho Afrika. Daud aliifungia Yanga bao la kwanza katika sekunde ya 27 tu ya mchezo, likiwa ni bao la mapema zaidi kwenye michuano hiyo msimu huu. Bao hilo linatengeneza rekodi kwa Daudi na Yanga kwa ujumla kutoa mchezaji aliyeweza kucheka na nyavu ndani ya nusu dakika dhidi ya Wolaitta Dicha SC kutoka Ethiopia. Yanga iliibuka na ushindi wa jumla ya mabao 2-0 katika mchezo uliopigwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam jana. Bao jingine la Yanga lilifungwa na Mshambuliaji Emmanuel Martin kwa njia ya kichwa katika dakika ya 54 ya kipindi cha pili. Matokeo hayo yameifanya Yanga kujitengenezea mazingira mazuri ya kuingia hatua ya makundi katika mchezo wa marudiano utakaopigwa wiki moja baadaye huko Ethiopia.
Kocha wa Juventus, Massimiliano Allegri amemfananisha Cristiano Ronaldo na kinywaji cha mvinyo akisema kuwa kadiri umri unavyokwenda ndio anazidi kuwa mkali zaidi. Allegri alimkubali Ronaldo baada ya kuiongoza Real Madrid kuirarua Juventus 3-0 mbele ya mashabiki wao kwenye mechi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, wiki iliyopita. “Unajua Ronaldo yaani ni sawa na mvinyo kadiri muda unavyokwenda ndio anazidi kuwa bora,” alisema Allegri baada ya mchezo huo, ambao Ronaldo aliacha mashabiki wa soka mdomo wazi baada ya kufunga bao maridadi la ‘tik tak’. Allegri alisema kuwa Ronaldo amekuwa straika bora wa dunia kwa miaka miwili sasa. Alisema kuwa pamoja na fowadi huyo kuwa na umri wa miaka 33 lakini bado ana kiwango cha kutisha. Nyota ya Ronaldo bado ipo juu Real Madrid wakati wenzake waliounda kombinesheni ya BBC yaani Gareth Bale na Karim Benzema wakiwa wamechuja siku za karibuni. Katika miaka ya nyuma, Ronaldo alikuwa anasifika kwa mbio na chenga lakini kutokana na umri kumtupa mkono siku hizi anahakikisha anakuwa kwenye nafasi nzuri ya kufunga kila mara.
Ligi Kuu Soka Tanzania Bara inaendelea tena Jmapili ya leo kwa viwanja vinne kuwaka moto. Mechi kubwa inayosuburiwa mjni Mbeya katika Uwanja wa Sokoine ni Mbeya City watakaokuwa wenyeji watakuwa wanaikaribisha matajiri wa jiji la Dar es Salaam, Azam FC, mechi itaanza saa 10 kamili jioni. Mechi zingine zitakazopigwa leo ni:- Stand United vs Njombe Mji FC - Kambarage Stadium (Saa 10 jioni) Ndanda FC vs Kagera Sugar - Nangwanda Sijaona (Saa 10 jioni) Ruvu Shooting vs Tanzania Prisons - Uwanja wa Mabatini (Saa 10 jioni)
Na George Mganga Kufuatia kukosekana katika mchezo wa Kombe la Shirikisho jana dhidi ya Wolaitta Dicha FC kutoka Ethiopia, wachezaji Papy Kabamba, Obrey Chirwa, Kelvin Yondan na Said Makapu watakuwepo kwenye mchezo wa marudiano.
Wachezaji hao ambao wamekuwa mhimili mkubwa wa kikosi cha Yanga kwa msimu huu, walishindwa kutumika jana kutokana na kutumikia adhabu ya kadi mbili za njano kwa kila mmoja. Shirikisho la Soka Afrika (CAF), liliwatumia barua Yanga kuelekea mechi hiyo likiwakumbushia kutowatumia wachezaji hao sababu ya kadi hizo za njano. Tayari wameshamaliza adhabu hiyo waliyoitumikia jana, sasa watakuwa chachu ya kuongeza nguvu kwenye mchezo wa marudiano utakaopigwa nchini Ethiopia wiki moja baadaye. Yanga itaondoka nchini katikati ya wiki kuelekea Ethiopia kwa ajili ya mechi hiyo ambayo itakuwa ni ya mkondo wa pili. Kikosi hicho kitahitaji sare ama suluhu ama ushindi wa aina yoyote ile ili kusonga mbele kuingia hatua ya makundi.
Kiungo wa Yanga, Thabani Kamusoko amewapia wapinzani wao Wolayta Dicha wa Ethiopia katika mchezo wao wa leo kwa kusema wamejiandaa vilivyo kuwafunga.
Yanga leo Jumamosi inacheza na Dicha katika mechi ya kuwania kufuzu hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho baada ya kutolewa katika Ligi ya Mabingwa. Kamusoko raia wa Zimbabwe na wachezaji wenzake wamepania kuifunga Dicha katika mchezo huu wa kwanza wa mtoano wa Kombe la Shirikisho. Kama Yanga itaitoa Dicha na kutinga makundi kwenye michuano hiyo, itakuwa ni mara ya pili ndani ya misimu mitatu kwani katika msimu wa 2015/16, timu hiyo iliishia kwenye hatua hiyo. Akizungumzia maandalizi yao kuelekea mchezo huo wa leo, Kamusoko alisema: “Michuano ya Caf ukiangalia ni migumu na ina mazingira magumu sana ya kusonga mbele kutokana na jinsi ilivyo. “Ukiangalia kwa hatua hii tuliyofikia timu ikicheza mechi mbili na kushinda basi inaingia makundi, kitu hicho usichukulie rahisi, unatakiwa kufanya kazi kweli. “Sisi tumejiandaa vizuri na tunawajua wapinzani wetu wapo vipi, tunajipanga kufanya vizuri kuhakikisha tunaingia tena hatua ya makundi. “Tunawaomba mashabiki wetu waje kwa wingi kuisapoti timu yao kwa sababu wasipoisapoti itakuwa ngumu kwetu kufanya vizuri kwani tunajiona kama tunachokifanya si kizuri na hakiwapendezi wao mashabiki.” CHANZO: CHAMPIONI
Na Ibrahim Riyad Kuelekea mchezo wa Leo dhidi ya Simba, Uongozi wa Njombe Mji umesema timu yao ipo tayari kwa mapambano. Katibu Mkuu wa timu hiyo, Obed Mwakasungura, amesema wameshajiandaa kikamilifu kwa ajili ya kuikabili Simba. Aidha, Mwakasungura amewaomba mashabiki wa Njombe Mji FC kujitokeza kwa wingi kesho ili kuipa hamasa timu yao. Mwakasungura anaimani watapambana ili kupata ushindi leo japo amekiri kuwa mchezo utakuwa mgumu kwa kuwa kila timu imejipanga.
Msanii nyota Diamond Platnumz leo amepata fursa kuimba mbele ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli mapema leo jioni wakati wa hafla ya uzinduzi wa ujenzi mradi wa radar nne leo, ambapo pia Rais Magufuli alipokea ndege mpya aina ya Bombadier Q400.
Majina ya Blog Zinazoanzia na Herufi A
-
*1 .A Taste of Tanzania*
tasteoftanzania.com/blog
*2. Abood Msumi Network*
aboodmsuni21.blogspot.com
*3. Ahbaabur Rasuul*
ahbaabur.blogspot.co...